Karibu Mtukufu Ramadhani
Karibu Mtukufu Ramadhani
Mwenyezi Mungu (s.w.) anatufahamisha katika Qur’an
Karibu Mtukufu Ramadhani
Mwenyezi Mungu (s.w.) anatufahamisha katika Qur’an
Lakini hakuwahi kufika Mtwara…
Alikamatwa 2017 ameachiwa juzi
Na Bakari Mwakangwale
Mwaka mmoja wa Rais Samia ofisini
Na Shaban Rajab
Rais Samia Suluhu Hassan, aliapishwa rasmi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku ya Ijumaa ya Machi 19, 2021 katika Ikulu ya jijini Dar es salaam. Kuapishwa kwake kulimfanya kuweka historia ya Rais wa kwanza mwanamke nchini.
Rais Samia aliapishwa kushika wadhifa huo baada ya kifo cha mtangulizi wake Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Kabla ya kifo cha Dkt. Magufuli, mama Samia alikuwa Makamu wa Rais.
Kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, Rais Samia atahudumu kwa kipindi kilichosalia cha muhula wa urais hadi pale uchaguzi mwingine wa urais utakapofanyika 2025.
Machi 19, 2022, yaani wiki ijayo Rais Samia atakuwa anatimiza mwaka mmoja tangu kuapishwa kwake kushika wadhifa huo.
Mara baada ya kuapishwa, katika mambo ya awali kabisa kuyafanya akiwa Rais, na bila shaka hili lilikuwa ni kipaumbele chake cha kwanza, ni kuifungua nchi na kujenga mahusiano ya diplomasia ya kiuchumi.
Tunakumbuka ziara yake ya kwanza akiwa Rais, alizuru Uganda. Hii ilikuwa Aprili 11, 2021 ambapo alikutana na mwenyeji wake Rais Yoweri Museveni wa Uganda.
Akielezea lengo la ziara yake, alisema ni kuimarisha uhusiano wa nchi mbili na kumaliza makubaliano ya mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka nchini Uganda. Uganda na Tanzania zilisaini mikataba mitatu yenye nia ya kuendeleza sekta ya mafuta na gesi ya Uganda, wakati wa ziara hiyo.
Baada ya kumaliza kuzuru Uganda na kujihakikishia utekelezwaji wa mradi huo ambao unakuja kuwa na manufaa makubwa ya kiuchumi kwa nchi, Mei 2021 Rais Samia alizuru nchi jirani ya Kenya, lengo lilikuwa ni kurejesha mahusiano mazuri ya kibiashara na nchi hiyo jirani, ambayo yalishavurugika.
Ziara ya Samia nchini Kenya imechangia sehemu kubwa kufungua milango ya kibiashara kati ya nchi mbili jirani na kuondoa dhana na hofu zilizokuwepo ambapo uhusiano kati ya nchi hizo mbili ulikuwa ukizidi kudorora. Kupitia kauli zake katika kila fursa aliyopata kuzungumza, Rais Samia alisisitiza umuhimu wa mataifa hayo mawili kushirikiana bila kuwepo ushindani, kauli au vitendo vya kukwazana.
Katika ziara hiyo, Rais Samia aliahidi kuwa katika uongozi wake atahakikisha kuwa Kenya inabaki kuwa ndugu, jirani, mshirika wa mkakati ambao utafanya uhusiano kati ya nchi hizo mbili umefungwa katika mambo matatu.
Aliyataja mambo hayo kuwa ni undugu wa damu ambao hauwezi kutenganishwa na mipaka ya kuchorwa kwenye ramani, suala la kihistoria na kijiografia.
"Ushirikiano wetu si wa hiari, bali wa lazima kutokana na kanuni ya uasili wa undugu ambao Mwenyezi Mungu ameuumba, ushirika na ujirani yote yanatufanya tuwe pamoja na hatuna uwezo wa kulibadilisha. Kilichobaki ni tupendane au tuchukiane hatuwezi kukwepa kutokana na mambo haya matatu yaliyowekwa pamoja, tunategemeana kwa kila hali iwe kheri au shari." Alifafanua zaidi.
Rais Samia alisema lengo lake ni kuhakikisha kwamba wawekezaji wa kigeni wanajenga imani ya kuwekeza nchini Tanzania na ili kurahisisha hilo serikali imeanzisha miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo ya miundo mbinu kama barabara, reli , bandari na kawi, ili kupunguza gharama ya kufanya biashara.
Rais Uhuru Kenyatta, kwa upande wake aliahidi kuwa nchi zote mbili zitachukua hatua ya kuhakikisha kwamba makubaliano yote yaliyoafikiwa na Mawaziri wa Biashara wa nchi zote yanatekelezwa
Rais Kenyatta aliongeza kwamba Mawaziri hao watakutana katika kipindi cha wiki nne zijazo ili kujadili kuondolewa kwa vikwazo visivyo vya kodi ambavyo vinaathiri biashara kati ya Kenya na Tanzania.
Akihutubia kongamano la wafanyabiashara kabla ya kwenda Bungeni, Rais Samia aliwaambia wafanyabiashara hao:
"Mna bahati kwamba nchi zetu mbili upande mmoja kuna Uhuru wa kufanya biashara na upande mwingine kuna Suluhu ya kuondosha vikwazo vya biashara."
Kauli yake hiyo ilitazamwa kama juhudi yake binafsi kuhakikisha kuwa vikwazo vilivyokuwepo vilivyokuwa vinaathiri ushirikiano kati ya Kenya na Tanzania, vinashughulikiwa na kuondolewa ili kuwepo biashara huru kati ya nchi hizo mbili.
Katika Bunge la Kenya, Rais Samia alifafanua kuwa ziara hiyo ya kiserikali ya siku mbili nchini Kenya ilikuwa yake ya kwanza tangu aapishwe kuwa Rais wa nchi hiyo jirani, akisema ziara ya mwezi uliopita nchini Uganda haikuwa ziara ya kiserikali, bali ni ilikuwa ya kusaini mikataba ya kibiashara.
Kikubwa zaidi ambacho kiliwafurahisha wengi, ni hatua ya Kenya kutangaza kwamba Watanzania sasa hawatalazimika kuwa vibali vya kuruhusiwa kufanya kazi nchini Kenya.
Rais Samia katika hotuba yake na wafanyibiashara wa Kenya alisema taifa lake litathmini mambo yote yanayofaa kufanywa, ili kuhakikisha kwamba utaratibu wa kuwekeza ama kufanya kazi nchini Tanzania unarahisishwa.
Alisema Tanzania kwa sasa imetekeleza mageuzi kadhaa ili kuhakikisha kwamba biashara inaboreshwa ; mageuzi hayo ni kutathmini upya kodi na vikwazo visivyo vya kodi, kurahisisha utoaji wa vibali vya kufanya kazi kwa wawekezaji wa kigeni, kutathmini kodi na ada zinazotozwa kwa biashara na watu, usimamizi mzuri wa mfumo wa kodi, kuimarisha vita dhidi ya ufisadi hasa katika sekta ya utumishi wa umma, kufanikisha oparesheni za Ofisi ya pamoja ya kushughulikia biashara na uwekezaji na kupeana ardhi ya kutumiwa kwa uwekezaji.
Aidha walikubaliana, pamoja na mipango mengine, maendeleo ya mradi wa usafirishaji wa gesi asilia kutoka Tanzania hadi Kenya, vizuizi visivyo vya ushuru kati ya nchi hizi mbili kuondolewa ili kurahisha biashara na urahisi wa kusafiri katika kukuza utalii.
Juhusi za Rais Samia pia ziliwezesha kukubaliana kuharakisha utekelezaji wa mtandao wa usafiri wa anga, reli, baharini na wa barabara, na pia kuongeza ushirikiano katika utamaduni, sanaa, ujumuishaji wa kijamii na urithi wa kitaifa.
Marais hao pia walizungumzia kuboresha miundombinu ya barabara, hususan ujenzi wa barabara ya kutoka Malindi katika pwani ya Kenya mpaka Bagamoyo katika Pwani ya Tanzania.
"Pia tumesema tutaweka kipaumbele cha kuharakisha barabara kutoka Malindi, Lungalunga mpaka tufike Bagamoyo. Pia tutaanzisha safari za Ziwa Victoria wakati wananchi na mizigo inayopita kutoka Jinja, Kisumu, Mwanza Bukoba, ili kurahisisha biashara za wananchi wetu," amesema Rais Kenyatta.
Kwa ujumla katika ziara hiyo wakuu hao wa nchi walisisitiza kujitolea kwao kuendelea kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika sekta mbalimbali kama biashara na uwekezaji, madini, nishati, mifugo, uchukuzi, ulinzi na usalama, pamoja na kupambana na ugaidi na uhalifu uliopangwa kimataifa, kwa faida ya pande mbili za nchi hizi na watu wao.
Rais Uhuru Kenyatta, katika hatua ya kumhakikishia mgeni wake nia yake ya kuzuia kabisa uwezekano wa biashara kati ya nchi hizo kuvurugika, aliagiza maafisa wa serikali kuhakikisha kwamba mahindi yaliyozuiliwa mipakani kutoka Tanzania yanaruhusiwa kuingia Kenya.
Bila shaka uamuzi huo wa Kenyatta ulileta faraja kwa Watanzania, ambako wakulima na wafanyabiashara walikuwa wanategema soko la Kenya kuuza nafaka zao.
Itakumbukwa mapema mwezi Machi, Kenya ilipiga marufuku ununuzi wa mahindi kutoka Tanzania. Uamuzi huo ulifikiwa ikidaiwa kwamba baada ya uchunguzi ilibainika kwamba mahindi kutoka Tanzania sio salama kwa matumizi ya chakula cha binadamu.
Aidha ziara ya Rais Samia nchini Kenya uliweka sawa ushirikiano katika upimaji na uzuiaji wa kusambaa kwa virusi vya corona, katika maeneo ya mipakani bila kuathiri biashara na utangamano wa watu kutoka nchi hizo mbili.
Hatua hiyo ilirahisisha shughuli za wafanyibiashara wa mipakani na madereva wa malori ya bidhaa ambao waliathiriwa sana na baadhi ya masharti ya kupambana na Corona kwa sababu ya kutokuwepo kwa mpango wa pamoja wa nchi hizo mbili kukabiliana na janga la Corona.
Mara moja walikubaliana na Rais Kenyatta kuwa na Tume ya pamoja ya mawaziri wa nchi hizo mbili, iwe inakutana mara kwa mara ili kutatua changamoto za kibiashara na uhusiano zinatazotokea.
Rais Samia pia alitumia ziara yake kumwalika Rais Kenyatta kuwa mgeni rasmi wakati wanasherehekea miaka 60 ya Uhuru mnamo Desemba.
Tunakumbuka Rais Samia pia alipigia chapuo zaidi lugha ya Kiswahili katika ukanda wa Afrika Mashariki.
“Tulifurahishwa sana na uamuzi wenu wa kuanza kutumia lugha ya Kiswahili bungeni. Hiyo ndiyo inayonifanya nisikilize vikao vya bunge la Kenya. Ninapenda Kiswahili chenu...ni burudani ya kutosha. Nilikuwa nikisikiliza wakati spika akijitahidi kutaja nambari za mwaka kwa Kiswahili.” Alipongeza Rais Samia na kuonyesha shukrani zake kufuatia uamuzi huo wa Serikali ya Kenya.
"Niwahakikishie, mimi na wenzangu nchini Tanzania tutahakikisha kuwa uhusiano wetu unang'ara na kwa kufanya hivyo tung'arishe uhusiano wa Afrika Mashariki. Tanzania itaendelea kuwa jirani mwaminifu wa Kenya na mwanachama muadilifu wa Afrika Mashariki," amesisitiza Rais Samia.
Endapo kuna kipimo cha kufahamu iwapo ziara ya Rais Samia nchini kenya ilikuwa na manufaa kwa nchi zote mbili, basi muda ndio utakaohitajika kukadiria utekelezwaji wa kauli, ahadi na sera ambazo viongozi hao wawili waliahidiana wakati wa mkutano wao wa siku mbili .
Wengi wanangoja kwa hamu kuona kasi itakayotumiwa na kila serikali ili kufanikisha urahisishaji wa taratibu za kufanya biashara na ushirikiano wa watu na serikali za Tanzania na Kenya .
Katika muendelezo huo huo wa kufufua na kuimarisha diplomasia ya kiuchumi, ndani ya kipindi chake cha mwaka mmoja cha uongozi wake, katika moja ya ziara zake za awali tangu kuingia madarakani, Rais Samia alizuru nchi ya Burundi.
Alikutana na mwenyeji wake Rais Evariste Ndayishimiye, jijini Bujumbura. Katika mazungumzo yao walikubaliana kukuza ushirikiano baina ya nchi zao katika sekta mbalimbali. Rais Samia aliahidi Tanzania itaendeleza juhudi zake kuhakikisha Burundi inaondolewa vikwazo vyote ilivyowekewa na jumuiya ya kimataifa.
Rais Ndayishimiye, alitoa shukran kwa Tanzania kwa kuwapa hifadhi wakimbizi wa Burundi huku akisema wamekubaliana kushirikiana kuzuwia kuenea kwa silaha ndogo ndogo katika nchi hizi mbili.
Rais Samia pia aliahidi kuwa uhusiano na ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili ujikite zaidi kwenye masuala ya kiuchumi na kibiashara, hivyo waliangazia jinsi ya kukuza uwekezaji na biashara kati ya nchi hizo mbili.
Matokeo yake, tayari mwekezaji kutoka Burundi anajenga kiwanda cha mbolea jijini Dodoma, ambacho kinadhaniwa kuwa kitahisisha upatikanaji wa mbolea nchini. Tunafahamu hivi sasa nchi inakabiliwa na uhaba mkubwa wa mbolea. Ujio wa kiwanda hiki utasaidia kwa kiasi fulani kupunguza uhaba huo, lakini pia kitasaidia kuongeza ajira na kuunguza kiwango cha uagizaji wa bolea nje ya nchi.
Lakini pia tayari Rais Ndyeshimye alizuru nchini kukabidhia eneo la kujenga bandari kavu kwa ajili ya bidhaa za Burundi kutika bandari ya Dar es Salaam kule Kwala, mkoani Pwani.
Lakini Marais hao pia walikubaliana kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa kuondoa vikwazo vya kodi na visivyo vya kodi. Ujenzi wa kituo cha huduma za pamoja utaharakishwa kwenye eneo la mpakani la Manyovu Mugina.
Rais Samia aliangazia pia sekta ya madini na kuelezea kwamba Burundi, ina hazina kubwa ya madini ya Nickel na Chuma katika mkoa wa Rutana, madini hayo yanapatikana pia Kabanga Tanzania. Hivyo watashirikiana katika uchimbaji na kutafuta soka la madini hayo.
Rais Samia alizuru Kiwanda cha Fomi kinachotengeneza mbolea za kisasa, ambao ndio wanaojenga kiwanda kingine Dodoma na akaitembelea Benki ya Tanzania CRDB tawi lake la Burundi.
Desemba 7, 2021 Rais Samia Suluhu Hassan, alihudhuria hafla ya kuzindua Kiwanda cha Kutengeneza Vifaa vya Umeme cha Elsewedy Electric East Africa Limited, kinachomilikiwa na mwekezaji kutoka Misri.
Makundi ya wawekezaji yanayowasili nchini, ni matokeo ya ziara yake aliyoifanya nchini Misri.
Aliwataka Watanzania kuwapokea vizuri wawekezaji ili waingie nchini kujenga ustawi wa uchumi na kuzalisha ajira.
Aliahidi kuwa serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji na kuboresha sheria na sera ili zitabirike na zisibadilike mara kwa mara.
Kundi hilo la wawekezaji limejitokeza kabla ya kukamilika mwezi mmoja tangu akutane na kuzungumza nao nchini Misri.
Kiwanda hicho kinaelezwa kuwa ni kikubwa kuliko vyote Kusini mwa Jangwa la Sahara na kitawezesha Tanzania kuuza bidhaa nje ya nchi na kuingiza fedha za kigeni.
Ilieleza kiwanda kitazalisha mita 100,000 za nyaya na Transoma 15,000 kwa mwaka na kwamba uwekezaji huo ni kielelezo sahihi fursa nyingi zilizopo nchini.
Mbali na mambo mengine, kiwanda hicho kitapunguza utegemezi wa kuagiza bidhaa kutoka nje na badala yake chenyewe kitauza bidhaa nje ya nchi.
Aidha ilifahamishwa kuwa mpango wa mwekezaji huyo ni kujenga chuo kitakachofundisha Watanzania namna ya kufanya kazi ili waajiriwe katika kiwanda hicho.
Serikali inaendelea na mpango wake wa ujenzi wa Chuo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na muda wowote jengo linaanza kujengwa.
Ziara ya Rais Samia kwenda Misri ilikuja na matunda ya wafanyabiashara wakubwa 40 wanaohitaji kuwekeza kwa kuanzisha viwada 40 nchini.
Ukiacha ziara za kuifungua nchi na nchi jirani, Lakini jambo jingine lenye afya sana kwa Watanzania alilolifanya kwa Taifa letu ni kitendo chake cha kuiamuru TRA kufungua akaunti za watu zilizokuwa zimefungwa.
Itakumbukwa mwezi Mei, 24 2021Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitangaza kuzifungulia akaunti zote za watu na wafanyabiashara ilizozifungia kwa sababu mbalimbali.
Hata hivyo, taarifa ya TRA ilisema fedha zilizokuwamo kwenye akaunti hizo kabla ya kufungiwa, hazitarejeshwa kwa wahusika kwa kuwa zilitumika kulipa madeni wanayodaiwa na taasisi za Serikali.
Kauli hiyo ya TRA ilikuja baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuonya kitendo cha kufunga akaunti na uonevu dhidi ya wafanyabiashara kinawafanya wahamie nchi nyingine kuendeleza biashara zao.
Awali Rais Samia alitoa kauli hiyo Aprili mosi mwaka huu, baada ya kuwaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, huku akimtaka Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba, kutanua wigo wa ukusanyaji kodi na kuongeza walipa kodi wengi zaidi.
Kwa takriban miaka mitano kulikuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wafanyabiashara kuhusu akaunti zao kufungwa na fedha zao kuchukuliwa na TRA au taasisi za Serikali ili kufidia madeni wanayodaiwa.
Wafanyabiashara pia walilalamikia kikosi kazi ‘task force’ cha TRA kilichopewa majukumu ya kufuatilia madeni ya kodi kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali. Kikosi hicho kazi kinadaiwa kuchukua fedha katika akaunti za wahusika bila kufanya mazungumzo huku wafanyabiashara wengine wakidai fedha zao kuchukuliwa kwa uonevu.
Pamoja na Rais Samia ndani mwaka mmoja wa uongozi wake kurejesha imani ya wafanyabiashara na wawekezaji kwa serikali, lakini kuna jambo kubwa zaidi ambalo ndani ya uongozi wake limefanyika na kurejesha furaha za Watanzania.
Jambo lenye ni juu ya kujali haki za watu na kuichukia dhulma. Itakumbukwa mwezi Juni 2021 , Viongozi wa Jumuiya za Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI), Sheikh Farid Hadi Ahmed na Mselem Ali Mselem waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya ugaidi waliachiwa huru.
Aidha baadae watuhumiwa wengine waliokuwa wameunganishwa nao waliaondolewa mashtaka yao na kuwa huru.
Wawili hao na wenzao wengine ambao walikuwa mahabusu tangu mwaka 2014 kutokana na kukabiliwa na mashtaka hayo ambayo hayana dhamana, waliachiwa huru baada ya DPP kuwafutia mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili.
Washtakiwa hao walikuwa wanatuhumiwa kujihusisha na makosa ya ugaidi kinyume na kifungu cha 27(c) cha sheria ya kuzuia ugaidi ya 2002 Januari 2013 na Juni 2014.
Lakini hadi sasa tumeendelea kushuhudia watuhumiwa wengine waliokuwa wakishikiliwa, hususana viongozi na waumini wa Kiislamu wanaendelea kuachiwa huru kwa awamu kutoka mahabusu za magereza mbalimbali nchini na kufutiwa mashtaka yao. Tumesikia wakiendelea kuachiliwa huru huko Mtwara, Tanga na Arusha. Hii ni dalili ya dhahiri kwamba, Rais Samia na serikali yake inaonyesha dalili za wazi za kulinda haki za watu.
Kama haitoshi mapema mwezi huu wa tatu, Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na mMaendele CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe, naye ameachiwa huru na kufutiwa mashtaka ya ugaidi yaliyokuwa yamefunguliwa dhidi yake.
Na baada ya kutoka Rais Samia akaonana naye na kuzungumza. Yote haya ni ishara kwamba, Kiongozi aliyepo ana hofu ya Mungu na ana Imani.
Pamoja na kusakamwa kwa kukopa, Rais Samia, Oktoba mwaka jana alizinduza Mpango wa Serikali ya Tanzania wa kuinua Uchumi kwa kutumia mkopo wa fedha wa shilingi Trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) na kukabiliana na ugonjwa wa virusi vya Corona.
Sehemu ya mkopo huo ilielekezwa katika kugharamia ujenzi wa madarasa, mradi ambao ulikamilika Desemba 15, 2021.
Madarasa hayo yamejengwa baada ya Ofisi ya Rais TAMISEMI kupokea mgao wa fedha za maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya Uviko-19 bilioni 535.68 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 12,000 ya sekondari na 3000 ya vituo shikizi.
Vyumba hivi vina uwezo wa kuchukua wanafunzi wote watakaochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2022.
Februari 16, 2022 Rais Samia, alifanya ziara ya kikazi ya siku kumi katika nchi za Ulaya na Arabuni. Ziara hiyo imefungua milango ya mahusiano ya kidiplomasia, kiuchumi na kijami, milango ambayo ilipigwa komeo katika kipindi cha utawala wa awamu ya tano.
Siku 10 za ziara hiyo zimefungua milango ya mahusiano ya kidiplomasia, kiuchumi na kijami, milango ambayo ilifungwa kwa 'kufuli la chuma' hapo awali.
Kipindi kile ambacho hatukuwa vizuri, walifikia hatua ya kuzuia fedha za miradi ambayo Tanzania iliomba, lakini sasa wamefungua na kila kitu kiko vizuri", amenukuliwa akisema Rais Samia, kwenye moja ya mahojiano yake kuhusu ziara hiyo.
Hasara za kufunga mlango wa mahusiano hasa na nchi za Umoja wa Ulaya, zilikuwa kubwa zaidi kuliko faida.
Kwa mujibu wa Rais Samia, amefanikiwa kupata fedha za msaada kiasi cha Euro milioni 450 sawa na Shilingi trilioni 1.17 kutoka Umoja wa Ulaya (EU) ikiwa ni sehemu ya Euro bilioni 55 zilizotengwa na Umoja huo kwa ajili ya Afrika kukabiliana na janga la Covid 19.
Katika kipindi cha cha miaka mitatu ijayo fedha hizo zitatumika kukwamua miradi iliyokwama ya viwanja vya ndege Kigoma, Shinyanga na Pemba, ukarabati wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Dar es Salaam (Terminal II), Mafunzo, mradi wa mabasi ya umeme, ukamilishaji wa mradi wa mabasi ya mwendo wa haraka na kilimo.
Euro milioni 450 ni fedha zinazoweza kuchochea maendeleo ya nchi kwa kasi. Uwepo wa fedha hizi na zikasimamiwa vyema, mbali na malengo yake ya moja kwa moja, utaongeza pia mzunguko wa fedha mtaani na kuchangamsha shughuli za uchumi kwa wananchi.
Shughuli za uchumi zikichangamka, unatengeneza ajira na kuongeza kipato cha watu, mwishowe unaboresha maisha yao kwa sababu wataweza kumudu kununua bidhaa, huduma na mahitaji muhimu kuendesha maisha yao.
Mwishoni mwa mwaka jana Tanzania ilipokea mkopo wa shilingi trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF), kwa ajili ya kushughulikia janga la Corona. Mkopo huu umesaidia ujenzi wa maelfu ya madarasa nchi nzima na kutafsiri vyema mpango wa serikali ya Tanzania wa kuinua uchumi wake na wa watu wake. Kama zilivyo kwa fedha hizi, fedha za 'Ulaya' alizozipata Rais Samia kama zitatumika vyema, zitasaidia kuinua sekta lengwa.
Tarehe 17 Februari, 2022 Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza na Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo ya Ubelgiji, Luxembourg, Afrika, Caribbean na Pacific (CBL-ACP), Brussels nchini Ubelgiji leo
Katika kipindi cha miaka sita iliyopita Tanzania ilisakamwa kwa kutokuwa na mahusiano mazuri kidiplomasia na Jumuia au na nchi nyingine. Rais aliyemtangua, Hayati Dkt. Magufuli, alipendelea kutuma wawakilishi katika mikutano mingi mikubwa na hakuwahi kusafiri kwa ziara yoyote ya kikazi nje ya bara la Afrika.
Hata kwa ziara zake ndani ya Afrika, alizuru nchi tisa tu kati ya nchi zaidi ya 50 katika wakati wote huo, akitembelea nchi za Rwanda, Kenya, Ethiopia, Burundi, Uganda, Afrika Kusini, Namibia, Malawi na Zimbabwe.
Lakini katika kipindi cha chini ya mwaka mmoja Rais Samia, ameshatoka kwa uwiano mara nyingi zaidi ya mtangulizi wake. Na safari hii akienda Ulaya ambapo uhusiano wa Jumuia ya bara hilo na Tanzania umedumu kwa miongo zaidi ya mitano.
Rais Samia mwenyewe alikiri kwamba katika kipindi hicho uhusiano wa Tanzania na Jumuia ya Ulaya ulikuwa na changamoto.
"Wakati ule ulikuwa ni mtazamo, tulikuwa tunaangalia mambo ya EPA (Mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi), kulikuwa kuna kugongana gongana kwenye ideology kwenye siasa, labda Ulaya walisema jambo ambalo halikutupendeza, lakini baada ya muda tumezungumza na yote yako sawa sasa", alinukuliwa Rais Samia.
Haki inayotajwa kukiukwa wakati wa utawala uliopita ni pamoja na vyama vya siasa kutofanya mikutano siasa kama inavyotakiwa, ingawa hali hiyo inaonekana kuwepo sasa, lakini mkazo wake haufanani na sura ya wakati ule.
Mbali na fedha, ziara ya Rais Samia Ulaya, imefungua ukurasa mpya wa uhusiano wa kidiplomasia baina ya taifa hilo na Jumuia ya Ulaya baada ya dhana ya 'mabeberu' kufifisha uhusiano wa pande hizi mbili kwa miaka mitano.
Tunakumbuka kabla ya kuingia kwa awamu ya tano ya uongozi wa serikali, Uhusiano wa Umoja wa Ulaya na Tanzania, haukuwa na changamoto nyingi. Ni katika awamu hii dhana ya wageni kutoka mataifa mengi ya kigeni kuonekana 'mabeberu' iliposhika kasi na kuonekana kama watu wenye mitazamo ya kunyonya zaidi kuliko kusaidia.
Hata kama dhana hiyo ilikuwepo nyuma, namna ilivyobebwa iliongeza wigo wa utofauti wa mitazamo katika sera, mipango na maoni.
Leo ubeberu, sio hoja, Rais Samia amewakaribisha na anawafuata walipo na maisha yanaendelea.
Ubeberu na mabeberu, tunaweza kuiona ni ya dhana ya maana, lakini kiuhalisia, ubeberu ni falsafa ambayo inakutegemea unalindaje maslahi ya nchi katika kulinda rasilimali na watu wako dhidi ya hao wanaoitwa mabeberu.
Tangu aingie madarakani, Rais Samia amekuwa akifanya ziara mara kadhaa na kuhudhuria mikutano ya kimataifa ambayo inaweza kuwa ni fursa kwa nchi.
Tumeshuhudia, faida kubwa ya kufanya hivyo katika kipindi cha mwaka mmoja tu tangu aingine madarakani Machi 19, 2021.
Liko wazi kwamba Rais Samia anaaamini katika kujenga na kudumisha mahusiano ya kidiplomasia na mataifa na jumuia nyingine. Amekuwa akifanya vikao vingi na kukutana na viongozi mbalimbali wa mataifa ya Afrika na nje ya Afrika pamoja na mashirika ya kimataifa.
Pamoja na muelekeo huo, Rais Samia, hatapimwa kwa idadi ya ziara zake nje ama amekutana na watu wangapi, atapimwa kwa matokeo ya ziara hizo, ikiwemo hii aliyokutana pia na Rais wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen, nchini Ubelgiji.
Hivi karibuni tumeshudia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetia saini Hati za Makubaliano (MoU) 36 wakati wa mkutano wa Biashara na Uwekezaji uliofanyika Dubai.
Hati 12 kati ya hizo zimetiwa saini baina ya serikali ya Tanzania kupitia wizara na taasisi za umma na wawekezaji mbalimbali wa sekta za umma na binafsi.
Vile vile, hati za makubaliano nyingine 23 zimetiwa saini baina ya makampuni binafsi kutoka Tanzania na makampuni mengine yenye nia ya kushirikiana katika sekta mbalimbali za kiuchumi.
Hati moja itahusisha Wizara ya Biashara na Viwanda ya Zanzibar na wawekezaji wanaonuia kushirikiana kwenye sekta ya utalii.
Idadi ya ajira zinazotarajiwa kupatikana kwa ujumla kutokana na makubaliano hayo ni zaidi ya 200,000 katika kipindi cha miaka minne, huku uwekezaji huo ukigharimu zaidi ya dola bilioni 7.49 ambayo ni sawa na shilingi trilioni 17.35 za Tanzania.
Sekta zinazotarajiwa kunufaika na hati hizo za makubaliano ni pamoja na nishati, kilimo, utalii, miundombinu, usafiri teknolojia na nyinginezo.
Akiongea katika mkutano huo wa Biashara na Uwekezaji, Rais Samia Suluhu Hassan alisema ili kushawishi uwekezaji na kutengeneza bidhaa madhubuti na za kisasa, nchi inahitaji elimu bora.
Ya kueleza ambayo yanaonyesha dalili nzuri mbele ya safari kwa uongozi huu wa awamu ya sita ni mengi, lakini tuseme tu kwamba, mwaka moja wa Rais Samia umeonyesha dalili nzuri kwa kiasi kikubwa, hususan upande wa haki na uwekezaji.
Anaweza asikamilishe kila tunalolitamani kwa sasa, tumpe muda maana bado anayo nafasi, miaka minne imesalia ya Awamu hii.
Waachiwa wakamatwa tena
Washtakiwa upya, warudishwa gerezani
Wamwaga machozi, wamekaa miaka 8 Mahabusu
Na Bakari Mwakangwale
Waongoza Waislamu katika Dua ya Kunuti
Mmoja akhutubu Mtambani, mwingine Masjid Jumaa
Na Bakari Mwakangwale
Na Bint Ally Ahmed
KITUO cha Andalusia Training Center ikishirikiana na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), wanatarajiwa kufanya kongamano kubwa kwa wanandoa hapa nchini.
Na Bakari Mwakangwale
JUMUIYA ya Wanataaluma wa Kiislamu Tanzania (TAMPRO), inatarajia kufanya Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa viongozi wapya wa Kitaifa, sambamba na kutoa sura mpya ya kiutendaji.
Ni baada ya kushinda shindano la Qur’an.
Na Bint Ally Ahmed
Group Khairat watoa msaada magereza Handeni, Maweni
Na Bint Ally Ahmed
Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu Tanzania, kupitia kundi la kina mama la mtandao wa Whatsup lenye anuani ya Groups Khairat, wametoa msaada wa chakula chenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja na laki tano (1,500,000) kwa wafungwa na mahabusu wanaotumikia vifungo vyao katika gereza la Handeni na gereza la Maweni Jijini Tanga, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu limekuwa linafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha wanawake wa Kiislamu nchini, linaloongozwa na Ukht. Fatma Ally Chitapa, ambaye pia ndiye kiongozi wa group hilo, limekuwa likiwaelimisha kina mama juu ya dini yao na dunia pia, lakini pia wamejikita kwenye malezi bora ya Kiislamu kwa kuwa mwanamke ndio msingi na nguzo ya familia.
Ukht. Fatma, amesema kuwa kundi lake la Whatsup linalotokana na Baraza Kuu la Wanawake wa Kiislamu hapa nchini, wamekuwa wakijihusisha na kusadia wahitaji mbalimbali kama vile vituo vya watoto yatima na wale wenye uhitaji maalumu na kutekeleza kazi zake mbalimbali za masuala ya kidini kwa kipindi kirefu.
Ukht. Fatma, ameongeza kuwa wamekabidhi chakula hicho kwa Mkuu wa gereza la Maweni, Revocatus Kessy, mchele kilo 300, mafuta ya kupikia lita 60, sabuni boksi kubwa moja, Misahafu ya Tafsiri pamoja na vitabu mbalimbali vya mafundisho ya dini ya Kiislam.
Baadae walikabidhi chakula hicho kwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Anthony Mbogo, kupitia kwa Mkuu wa Gereza la Handeni
mchele Kilo 200, mafuta ya kupikia lita 40, Sabuni boksi kubwa moja, Misahafu ya Tafsiri pamoja na vitabu mchanganyiko vya mafundisho ya Uislamu.
Aidha wafungwa hao nao walipata fursa ya kutoa neno la shukrani kwa wanawake hao na kujiona ni miongoni mwa watu wanao kumbukwa na jamii ya uraiani.
Group Khairat limekuwa likifanya kazi mbalimbali za kheri kwa kuchangishana kidogo walicho nacho na kukifikisha kwa wahitaji.
Kwa kuzingatia umuhimu wao wa kutoa kile walicho jaaliwa na Mola wao, kikundi hicho kila wanapoona kuna shida au uhitaji eneo fulani, huchangishana pesa na kuzipeleka pale wanapoona kuna uhitaji.
Mkuu wa gereza la Handeni, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Anthony Mbogo na mahabusu walitoa shukran zao za dhati kwa sadaka hiyo waliyoipokea kutoka kwa kina mama hao.
Alisema wafungwa na mahabusu pamoja na watumishi wenzake wanashukuru kwa kile kilichotolewa kwa ajili ya wafungwa.
Mkuu huyo wa gereza aliomba ushirikinao katika kutatua changamoto nyingine kama hizo.
Kwa upande wa Mkuu wa Magereza Wanawake Maweni, Upendo Kazumba, aliwashukuru kina mama hao kwa moyo wao wa kujali na kutoa walicho nacho kwa ajili ya wahitaji na kuwaomba kutowasahau hata kwa kidogo walicho nacho, kwani kutoa ni moyo na sio utajiri.
Msaidizi wa Kikundi hicho cha wanawake Ukht. Mayasa Sadalla, amesema kikundi kimetoa msaada huo kwa wafungwa wa gereza la Handeni na Maweni, Tanga kwa kuona kuwa wana jukumu la kuwakumbuka ndugu zao, hasa wathirika wa kesi za ugaidi wanaoshikiliwa mahabusu kwa muda mrefu sasa.
Ukht. Mayasa, amesema kuwa Baraza la Wanawake wa Kiislamu kupitia group la Khairat, waliguswa na kuona wana wajibu kufanya kila namna kuwasaidia wafungwa kwa kutoa walicho nacho, kwani kutoa ni moyo na kwa Allah hakuna kidogo.
Naye Ukht Fatma, amewaomba Waislamu kulikumbuka kundi hili la watu walioko magerezani, kwani wao wamesahaulika sana na jamii.
Kama una sadaka yako iwe ni magodoro, nguo za wanaume na wanawake, sabuni, mafuta kula, vitabu vya dini ya Kiislamu na mahitaji mengine muhimu ya mwanadamu na unahitaji kuifikisha kwa makundi mbali mbali yanayohitaji, unaweza kuwapigia kina mama hao wanao jishughulisha na mambo mbalimbali ya kheri katika jamii.
Wasiliana na Ukht. Fatma kwa namba hii 0712 326 612.
Na Bint Ally Ahmed
Taasisi ya Udugu Social Help Welfare yenye Makao Makuu yake Buguruni Jijini Dar es Salaam imefanikisha nia na matamanio yake ya kuwafariji yatima wa kituo cha Al-Azam kilichopo Mbagala, kwa kujumuika na watoto hao pamoja na walezi wao kwa kupata
Aidha, Taasisi hiyo imetoa wito kwa wadau kuendelea kuwakumbuka na kuwajali yatima na watoto wanaoishi katika mazingira magumu popote walipo, kwani bado wanazo changamoto nyingi zinazohitaji ufumbuzi.
Akizungumza mara baada ya kupata chakula cha mchana na yatima hao, mratibu wa kundi hilo lenye wanachama zaidi ya 20, Hajat Neema Maumba amesema kilichowasukuma kushiriki chakula pamoja na yatima ni kuwafariji, wasijione wapweke katika maisha yao kwa kukosa malezi ya wazazi wao.
Amesema, ni utaratibu wao wa kila mwaka kushiriki chakula na watoto yatima na wamekuwa wakifanya hivyo katika maeneno mbalimbali katika jiji la Dar es Salaam.
Amesema taasisi yao ya Udugu Social Help Welfare sio ya kidini, lakini wengi wao ni Waislamu, na kwamba wanasaidia watu mbalimbali bila kujali dini zao.
“Sisi tunaitwa Udugu Social Help Welfare, tupo Buguruni Malapa, tuko wakina mama 20, tulianza mwaka 2009, tumekuwa tukisaidia watu wenye mahitaji sehemu nyingi na bado tunaendelea kufanya hivyo,” alisema kioongozi huyo.
“Tumesikia changamoto watoto hawa wanazokutana nazo katika kituo hiki, baada ya watoto kueleza changamoto zao, tunamuomba Mwenyezi Mungu atuwafikishe tuweze kusaidiana”, amesema Hajjat Neema.
Amesema kuwa wametoa msaada kwa watoto hao jumla ya vitu vyenye thamani ya shilingi laki sita na elfu sitini na nane (668,000) msaada uliotoka mifukoni mwao kwa kuchangishana kila mwezi.
Hajjat Neema amewataka Waislamu, hasa kina mama kuwakumbuka wenye uhitaji maalumu kwa kuwasaidia na kuwapa faraja kuwahurumia na kuona wao ni sehemu ya jamii.
“Watoto kama hawa wanahitaji ukaribu wetu, hivyo kushirikina nao ni kuwapa upendo ambao nao kama wanaadamu wanauhitaji sana,” amesema Hajjat Neema.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa taasisi ya kulelea watoto yatima na wenye mazingira hatarishi cha Al-Azam Orphanage Center Sheikh Musa Chele ametoa wito kwa wafadhili kuacha kuwatumia watu wa kati kufikisha sadaka zao katika makao ya watoto yatima.
Amesema, kwa muda mrefu watu hao wa kati (Agent) wamekuwa wakitumia fursa hiyo vibaya kwa kujinufaisha wao wenyewe badala ya watoto yatima.
Akielezea historia ya kituo chao, Sheikh Musa alisema Kituo chao kimeanzishwa mwaka 2009 kikiwa na watoto 10, wavulana 5 na wasichana 5, hadi kufika mwaka 2021, walikuwa na watoto 60, kati yao wanawake 35 na wanaume 25.
45 kati ya watoto hao 60, wanaishi katika Kituo na wengine wanalelewa wakiwa majumbani mwao.
Amesema Kituo kinakabiliwa na changamoto nyingi, lakini kubwa ni huduma za afya, watoto wengi hawana bima za afya ili kuwasaidia kupata matibabu bila hofu.
Pia amesema kuna changamoto ya rasilimali fedha za kulipa pango la nyumba, ada za wanafunzi, na chakula, kwa mwezi wanalipa shilingi 300,000 fedha ambazo ni nyingi kwa uwezo wao.
Upande wa mafanikio amesema, Kituo kimeweza kununua kiwanja na kuwaomba wadau kuwajengea nyumba ili watoto wakaishi huko na kuepukana na adha ya kupanga.
"TUNAFANYAJE Ustadh kuhakikisha akina mama wa Kiislamu wanauishi Uislamu?"
"Ustadh tunafanyaje ili mabinti zetu wawe salama kiimani..."?
Hili ndilo jambo la mwanzo ambalo Ukhty Nadhira angekuuliza punde ukikutana nae. Innaa lillaahi wa innaa ilayhi raajiuun. Amerejea kwa Mola wake, Alhamdulillaah! Ametekeleza wajibu wake na amefikisha ujumbe.
Kwa mara ya kwanza nakutana nae akiwa ni mwanafunzi wa program ya kuwaandaa Walimu wa EDK kwa Madrasa na Shule za Msingi mwaka 2006 wakati huo tayari ni mama wa watoto watatu. Mpaka wakati huo Ukhty Nadhira alikuwa mzoefu kwenye harakati za kuelimisha akina mama na mabinti wa Kiislamu, lakini kila aposikia panasomeshwa, basi alikuwa tayari kuwa mwanafunzi; kwa takriban wiki 30 hivi tulikuwa nae kama mwanafunzi. Hakuishia kuwa mwanafunzi bali alihamasisha wenzake kuwa wanafunzi na akawa mwalimu wao.
Kwa kuthanini program ile, Ukhty Nadhira aliianzisha katika Madrasa Rahman Kinyerezi mahali ambapo palikuwa ndio Kituo cha cha harakati, wakikutana akina mama na kujifunza Uislamu na kulea mabinti zao kiakili na kiroho.
Ukhty Nadhira mbunifu wa program za kimalezi, muanzilishi na msimamizi, amewalea vijana wengi wa kike na wa kiume kupitia Daarul Uluumi Kariakoo ambapo palikuwa pakiendeshwa semina mbali mbali za kimalezi kwa vijana na wanafunzi wa Kiislamu kidato cha kwanza hadi cha sita na wanufaika wa program ile waliendelea kuhudhuria hata walipokuwa vyuoni!
Ukhty Nadhira alihamasisha, kusimamia na kushiriki makongamano ya akina mama wa Kiislamu kimkoa, kikanda na kitaifa akishirikiana na akina mama wengine wa Kiislamu. Tija ya makongamano haya ni pamoja na uwepo wa madrasa hai za akina mama na mabinti wa Kiislamu, uwepo wa shule za awali katika madrasa nyingi na kutoa ajira kwa vijana waliosomea ualimu.
Huwezi kumtaja Ukhty Nadhira kwamba alikuwa tajiri kuweza kuyafanya yote haya, lakini alijaaliwa uwezo wa ku-mobilize rasilimali na kuzielekeza zinapostahiki hivyo kujenga Imani ya kuaminiwa na kukabidhiwa amana bila tone la shaka.
Tunamuadhimishaje Ukhty Nadhira?
Ukhty Nadhira alikuwa mpole sana kwa watu lakini mkali inapokuja jambo la Uislamu na Waislamu. Alikuwa mwenye msimamo akisimamia kile anachokiamini. Hakuwa mtu rahisi wa kukata au kukatishwa tamaa. Akipanga jambo lake muda wa kuwa anaamini yupo sahihi na lina tija kwa Uislamu na Waislamu, hachelei kubakia na watu wachache.
Alikuwa hodari mno wa kuwatia watu moyo na kuwapa bishara njema. Mwepesi kusaidia mwenye sikio makini na moyo laini. Aghalabu shida za watu wengine alizifanya zake.
Ameacha alama katika maisha ya akina mama na vijana wa kike na wakiume na kwa kila Imam na mwalimu wa madrasa aliyeshirikiana naye. Ni wajibu wetu kuendeleza pale alipoishia na kuongeza hima zaidi katika yale aliyoyafanya.
“Hao ni watu waliokwisha pita. Wao watapata waliyo yachuma, na nyinyi mtapata mliyo yachuma, wala hamtaulizwa nyinyi yale waliyo kuwa wakifanya wao.” (2:141)
Allah Ampe Kauli thabiti. Amrehemu na Amsamehe makosa yake.
Abu Sumayyah Salah
Na Bint Ally Ahmed
Waislamu wametakiwa kushukuru kwa kuachiwa huru Masheikh 36 wa Uamsho waliokuwa wakishikiliwa katika Gereza la jiji la Dar es Salaam, lakini wakatakiwa kuongeza
harakati za kupigania haki za idadi kubwa ya Waislamu na Masheikh wanaoendelea kushikiliwa kwa muda mrefu sasa katika magereza mbalimbali nchini.