Kaskazini “A” Unguja walilia maji
Na Salmin Juma, Zanzibar
Wananchi wa Shehia ya Chaani Masingini wilaya ya Kaskazini “A” Unguja wamesema wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha kutokana na kukosekana kwa huduma ya maji safi na salama baada ya kuanza ujenzi wa barabara iliyotoka Kwanyanya hadi Mkokotoni.