Walikuwa 61. Soma majina yao, Wapo Maimamu maarufu watatu
Walikamatwa na Polisi toka 2014
Na Bakari Mwakangwale
WAKATI kesi ya ugaidi inayowakabili Masheikh na Waislamu 59, waliopo katika gereza la Kisonge, Jijini Arusha, ikisubiri baraka za DPP, ili ianze kusikilizwa, watuhumiwa wawili wameshafariki dunia.
Awali kesi hiyo ilikuwa ina jumla ya Waislamu 61, sasa wamebakia Waislamu 59, kufuatia vifo vya Waislamu wawili, waliofikwa na umauti wakiwa watuhumiwa wa ugaidi, waliokuwa mahabusu gerezani wakisubiri hatma ya kesi zao.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kutoka Jijini Arusha, Waislamu waliofariki kwa nyakati tofauti ni Said Michael Temba na Morisi John, na miili yao kukabidhiwa kwa ndugu zao, ambapo mmoja alizikwa Jijini Arusha na mwingine Jijini Dar es Salaam, baada ya kuhamishiwa Hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu na mauti kumfika katika Hospitali hiyo.
Masheikh na Maimamu maarufu wanaosota gerezani kwa miaka saba sasa bila kujua hatima yao ni Sheikh Mohammed Said Ans (Sheikh Hambal), Jafari Lema pamoja na Sheikh Mustafa Kihago. Wote ni Maimam, ambao kwa ujumla walikamatwa na Jeshi la Polisi, mwaka, 2014.
Chanzo chetu cha habari kutoka ofisi ya RCO Jijini Arusha, kimelieleza Gazeti la An nuur, kuwa kwa sasa kesi hiyo inasubiri Waraka kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), pindi utakapofika kesi hiyo itaanza kusikilizwa.
Taarifa kutoka ofisi hiyo zimeeleza kuwa tayari maagizo yametolewa mikoani kote kwamba kesi zinazohusu tuhuma za ugaidi, zisikilizwe hivyo chanzo hicho cha habari, kimesema kwa sasa wao kama ngazi ya Mkoa, wanasubiri waraka wa DPP, ili waanze kusikiliza kesi hizo.
Itakumbukwa kuwa baadhi ya Waislamu na Masheikh hao walikamatwa kufuatia kutokea kwa milipuko kadhaa Jijini Arusha, ukiwemo ule uliotokea katika Kanisa la Olasiti, mwaka 2014.
Orodha ya majina ya Waislamu wenye tuhuma za ugaidi, waliopo mahabusu kwa miaka saba katika Gereza la Kisonge Jijini Arusha:
- ABDALLAH ATHUMANI LABIA
- SHABANI ABDALLAH WAWA
- ALLY HAMISI JUMANNE
- SUDI NASIBU LASUMA
- ABDALLAH JUMA NYAKWELA
- RAJABU PIRI HEMED
- ABDULRAZAQ MOHAMMED
- MAKA SUDI GEWE
- HASSAN ZUBERI SAID
- ALLY HAMISI KIDAHANYA
- SWALEHE HAMISI
- ABDALLAH YASSIN
- YASSIN HASHIM SANGA
- ABDALLAH MAGINGA WAMBURA
- ABDUL MOHAMMED HUMUD
- ATHUMANI HUSSEIN MMASA
- SHABANI MUSA MMASA
- MOHAMED NURU TEMBA
- SAIDI MICHAEL TEMBA (amefariki)
- JAFAL HASHIM LEMA
- MUSTAFA MOHAMED KIHAGO
- ABASHAR HASSANI OMAR
- HASSANI ABDALLAH OMAR
- YUSUPH ALLY HUTA
- YUSUPH ALLY ATHUMANI
- MALIJANI CHARLES MSWALI
- SHABANI IDD
- SWALEHE HASSANI OMARI
- SUMAIYA JUMA
- IDDY SALUM ABDALLAH
- YUNUS SALIM MSUTA
- YAHAYA TWAHIRU MPEMBA
- ABDUL HASSAN JUMA
- KIMOLO ISSA MSHANA
- IDDY RAMADHANI YUSUPH
- ABDULRAHMANI JUMANNE HASSAN
- ABDALLAH ABDULRHAMAN KIMORO
- AMANI MUSA PAKASI
- IBRAHIM LEONARD
- YASSIN MOHAMED SHABANI
- KASSIM IDRISA RAMADHANI
- HASSAN ALLY MFINANGA
- RAMADHAN HAMADI WAZIR
- HAMAD ISSA SIGHI
- ABDULRAMAN ABUBAKARI GICHA
- SAID OMARY SAID
- ANUARY NASHER HAYEL
- NIGANYA HAMIS NIGANYA
- MORIS JOHN (amefariki)
- BAKARI NTEMBO BILANGO
- RAJABU YAKUBU ABDALLAH
- ABDUL-AZIZ SHABANI MKINDI
- MOHAMED SAID ANS (SHEIKH HAMBAL)
- ISMAIL JUMA HUSSEIN
- MOHAMED SAID RASHID
- SADIC HUSSEIN
- MASUMAI FADHILI
- KHALID SHABAN
- BUCHUMI HASSAN
- JUMA SULEYMAN
- BAHARI LAZARO