Wafungwa wa Kipalestina wapo hatarini
Ni kwa kunyimwa chanjo
Chama cha Wafungwa wa Palestina kimetaka Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) kuweka shinikizo kwa utawala wa Tel Aviv, kuwaruhusu Wapalestina katika magereza ya Israel kupewa chanjo dhidi ya corona.
Chama hicho kimetoa madai hayo baada ya kufanya mkutano na waandishi wa habari mbele ya jengo la Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) katika Ukanda wa Gaza.
"Kuenea kwa haraka kwa janga la Covid-19 katika magereza kumesababisha hofu kubwa na wasiwasi kwa maisha ya wafungwa." Alieleza Bw. Ahmed al-Mudellel, Afisa wa Harakati ya Jihad ya Kiislamu, kwa niaba ya Chama.
Mudellel alisema kuwa hali ya kiafya ya wafungwa wa Kipalestina katika magereza ya Israeli iko hatarini kutokana na janga hilo na kwamba, Israel inakataa kuwapa chanjo wafungwa wa Palestina, na akautaka utawala wa Palestina kupeleka suala hilo katika ngazi za kimataifa.
Bw. Mudellel pia alitoa wito kwa Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) kuweka shinikizo kwa Israel kuruhusu matibabu na chanjo kutumika katika magereza.
Habari iliyochapishwa katika gazeti la Haaretz, ilielezwa kuwa Waziri wa Usalama wa Umma wa Israel, Amir Ohana, alituma maagizo kwa taasisi husika kutotoa chanjo ya Covid-19 kwa wafungwa wa Palestina katika magereza ya Israel.
Ilielezwa kuwa hadi sasa wafungwa 171 wa Kipalestina wamekutwa na Covid-19 katika magereza ya Israel.trt.net.tr.